Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Zainab Katimba, amemtaka Mkandarasi na Mtaalamu Mshauri anayetekeleza Mkataba wa Ujenzi wa miundombinu inayoratibiwa na mradi wa TACTIC wilayani Kahama Mkoani Shinyanga, kukamilisha haraka ujenzi huo kulingana na matakwa ya mkataba ili wananchi wanufaike kikamilifu na uwekezaji huo unaosimamiwa na Serikali kupitia TAMISEMI.
Saturday 1 November 2025
⁞
