#HABARI: Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, amedhamiria kuboresha miundombinu ya ufugaji ili wafugaji wafuge kisasa wakiwa katika maeneo yao rasmi na kuondokana na ufugaji wa kuhamahama.
Dkt.Kijaji amesema kufuatia mpango huo Wizara ya Mifugo na Uvuvi inadhamiria bajeti zake za fedha za kila mwaka zitoe vipaumbele kwenye malisho ya mifugo na maji ili kuwaondolea adha wafugaji kutotembea muda mrefu kufuata mahitaji hayo muhimu kwa ajili ya mifugo yao.
Sunday 2 November 2025
⁞
